Falsafa:
Gwajima awe Rais wa Tanzania mna mambo ya utani sana nyie...
Sio huyu Gwajima kwenye Jimbo la Kawe ndani ya CCM yake alipata kura 79 tu wakawachwa walioshinda akazawaidiwa ubunge na Magufuli? Kwa sababu alikuwa mshirika wa kuunda wasiojulikana?
Falsafa:
Samia ndio Rais wa nchi sasa na kutokana na udhaifu wa vyama vya upinzani mgombea Urais kutoka CCM ndio Rais wa nchi.
Je wananchi wepi waachiwe? Maana kiutaratibu chama ndicho kinatua ndio anapelekwa Kwa wananchi.
Kama unamwamini Mungu usimdhihaki.
Falsafa:
Maisha ya mtu ni kama alivyo ndani ya mawazo yake-Marcus Aurelius
Anayefanya chembe ya wema ataiona, na anayefanya chembe ya ubaya ataiona-Surat Az-Zalzalah 99:7–8
Maana aonavyo mtu katika moyo wake, ndivyo alivyo-Methali 23:7
Falsafa:
Kila mtu anajua kuwa Samia yupo hapo baada ya kifo cha Magufuli.
Na kawaida ya Rais kutoka CCM anakaa vipindi viwili hili kila mtu anajua Sasa Kikwete anahusika vipi? Lkn hata kama anahusika nchi gani inakwenda bila ushauri wa wazee?
Falsafa:
Chadema kutoka kuwa chama kikuu cha upinzani chenye lengo la kushuka dola, kuwa jukwaa la harakati ucharwa. Kila hoja wanadandia nyingi hazina maslahi na chama ila mtu binafisi kutaka kupata umaarufu (populist politics)
Falsafa:
2020 enzi za mtukufu wenu Magufuli ambaye alipata kunukuliwa akijiita malaika na watu wa karibu wakimuita Mungu hiyo fomu walichukuwa watu wangapi na kina nani?
Kama Magufuli alikuwa anapendwa kwanini walipora uchaguzi wa 2020?
Falsafa:
Je sio ole kwa yule anayetoa ole kwa wengine kwa maana ya kujipa mamlaka ya kutoka hukumu wkt naye anafanya dhambi na makosa?
Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi-Mathayo 7:1
Kwa maana kwa hukumu hiyo mhukumu nayo mtahukumiwa...Mathayo 7:2
Falsafa:
Kabla ya uchaguzi wa Chadema tulisema wengi wanaovuruga uchaguzi wa CDM sio wanachama wa CDM ila lengo lao kubwa kwa njia Moja au nyingine wanataka CDM ife.
Falsafa:
Sio Mama yetu ni Rais wa Tanzania usitake unataka yeye ndio amri jeshi mkuu wa nchi nafasi ya mamlaka ya juu kabisa kwenye nchi yetu.
Samia sehemu yupo hajajiweka mwenyewe ni kwa mujibu wa katiba.
Falsafa:
Enzi za Magufuli ni uoga gani ulipelekea Lissu kupigwa risasi?
Ni uoga gani kiongozi wa CDM Geita Alphonce Mawazo kuwawa kikatili enzi za JPM.
Ni uoga gari Ben Saanane kupotezwa baada ya kuhoji elimu ya mtukufu wenu?
Watanzania wanawazoom tu..
Falsafa:
Kutungwa sheria ni mchakato unaoanzia serikali wanapeleka bungeni mswada(bill) unajadiliwa na Wabunge wanaupitisha unapelekwa kwa Rais anatia sahini ndio unakuwa sheria.
Kwa maana halisi Wabunge hawatungi sheria maana wengi sio wataalamu wa sheria.
Falsafa:
Lema anapaswa kuwa mtu mzima sana hao CCM ambao wameongoza nchi Kwa 60+ tokea ikiwa TANU pamoja na mapungufu wameijenga nchi umesoma umekuwa mwanasiasa mpaka ukapata ukimbizi wa magumashi Canada.
Je wewe mwisho wako utakuwaje unaye hukumu wengine?
Falsafa:
Lissu na Lema ni wakimbizi wao na familia zao wanaishi kwa fedha za wafadhili
Wewe ulichelewa kuweka mpango ya kukimbia nchi 2021 na kupata ukimbizi kama mradi
Sasa unachokoza Mkuu wa nchi makusudi ili ushughulikiwe upate justification ya ukimbizi?
Falsafa:
Chadema chini ya Lissu kuna mambo mawili makuu.
1. Ina watu wa hovyo wasio na malengo.
2. Inatumika na dolla kijanja Kwa akili kubwa. NRNE ina faida Kwa CCM kutopata ushindani kwenye uchaguzi. Mambo yote ya CCM watu wa CDM ndio wanayatangaza zaidi.
Falsafa:
Wanaharakari pamoja na vyama vya upinzani vilipaswa kuikosoa serikali kusajili taasisi za dini ambazo nyingi zinaleta umasikini wa kufikiria kwa watanzania.
Huyu Pastor alipaswa kuungwa mkono kwa kujilipua kusema matapeli wa madhabau wapingwe pini
Falsafa:
Tulisema Chadema imetekwa na sio chama cha siasa Kwa sawa ni jukwaa la wanaharakari ambao wanatumia CDM kujitengenezea fedha kutoka Kwa wafadhini.
change.org sio taasisi ya kisiasa je ina mahusiani gani na CDM.
Je CDM Inatumika?
Falsafa:
Tukaneni mahakama na mamlaka kwa kuwa mna sehemu ya kukimbilia. Familia zenu zipo nje ya nchi zinakula kuku kwa mrija. Msipotanya hivyo mnapoteza uhalali wa kuwa wakimbizi.
Jambo baya mnatumia damu ya watanzania kwa maslahi yenu binafisi.